LORI LINGINE LA MAFUTA LATEKETEA KWA MOTO

Lori  jingine la mafuta aina ya Scania, lenye namba ya usajili T 243 BCU, na tela T 685 DCV mali ya kampuni ya Njombe Filling Station, limeteketea kwa moto baada ya kupata ajali katika Kijiji cha Ngadinda Halmashauri ya Madaba, Ruvuma.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma (RPC), Simon Maigwa Marwa, amethibitisha tukio hilo.

“Tukio la ajali ni kweli limetokea jana saa nne usiku (kuamkia leo Jumatatu) Songea Vijijini ambapo lori lilikuwa limebeba shehena petroli na likiendeshwa na Hubert Mpete ambaye bado hajajulikana alipo.  Lori hilo liliacha njia na kuingia porini kisha kugonga mti na kuwaka moto,  na kichwa (cabin) kiliungua chote,” alisema Marwa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post