GST YAENDELEA KUTOA ELIMU KWA UMMA NA WADAU WA SEKTA YA MADINI KATIKA WIKI YA MAONESHO YA VIWANDA SADC

Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) , yaendelea kutoa elimu kwa wadau wa sekta ya madini nchini katika maonesho ya wiki ya viwanda yanayoendelea katika mkutano  mkuu wa 39 wa  Nchi za Jumuhiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

 
Moja ya elimu inayotolewa na GST ni juu ya kazi za utafiti wa jiosayansi kwa maana ya jiolojia , jiokemia , jiofikia , miamba na madini nchini ikiwemo madini ya viwandani , madini nakshi (Dimension Stone), elimu nyingine ni juu ya uwepo wa madini ya ujenzi nchini.

Sambamba na elimu hiyo GST  ipo na machapisho mbalimbali ya  vitabu vya utafiti wa jiosayansi kama vile kitabu cha Madini yapatikanayo Tanzania toleo la nne  kitabu hiki kinaelezea uwepo wa madini kuazia ngazi kijiji mpaka taifa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527