GARI LA MKUU WA MKOA WA MARA ADAM MALIMA LAPATA AJALI LIKIDAIWA KUENDESHWA NA MTOTO WA DEREVA


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Juma Ndaki amesema gari la mkuu wa Mkoa huo, Adam Malima limepata ajali jana Jumapili Agosti 4, 2019 likiwa linaendeshwa na mtu anayedaiwa kuwa ni mtoto wa dereva wa mkuu huyo wa Mkoa.

Ndaki amesema ajali hiyo imetokea  jana saa 3 asubuhi na kwamba gari hilo lenye namba za usajili STL 5961 lilikuwa likiendeshwa na mtu ambaye taarifa za awali zinaeleza kuwa ni kijana wa dereva wa Malima.

"Mtoto na Baba yake wote wamelazwa Hospitali, Mtoto ana majeraha baada ya kupata ajali na gari ya Mkuu wa Mkoa na huyu baba ambaye ni Dereva wa Mkuu wa Mkoa alianguka kwa Presha tukamkimbiza Hospitali, maana alipata mshtuko bada ya kufika eneo la tukio na kuiona ajali"-Amesema


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527