BABA LEVO AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIEZI MITANO JELA


Msanii wa Bongo Fleva na Diwani wa kata ya Mwanga Kaskazini, Manispaa ya Kigoma Ujiji, Revokatus Kipando maarufu kwa jina la Baba Levo amehukumiwa kifungo cha miezi mitano kwa kosa la kumshambulia Askari wa Usalama Barabarani Mkoani Kigoma.

Inadaiwa kuwa  Baba Levo alimshambulia askari anayefahamika kwa jina la Msafiri Ponera, akiwa eneo lake la kazi eneo la Kwabela baada  ya  mtuhumiwa kulazimisha kupita kwa pikipiki wakati askari huyo akiwaruhusu watembea kwa miguu, na baada ya hapo Baba Levo aliamua kumshambulia askari huyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527