ALIYEKUWA MAKAMU WA RAIS ZIMBABWE AKIMBILIA MAFICHONI KUKWEPA KUKAMATWA


Makamu wa Rais wa zamani wa Zimbabwe ametangazwa na mamlaka nchini humo kama Mhalifu aliyekimbia.

Gazeti linalomilikiwa na serikali la Herald limesema kwamba Phelekezela Mphoko amekimbia kukamatwa na Kamisheni ya kupambana na rushwa nchini humo, ZACC.

Kiongozi huyo aliyekua madarakani mwaka 2014 hadi 2017 amekua akitafutwa ili kufunguliwa mashtaka ya matumizi mabaya ya ofisi pamoja na rushwa. 

Aliwahi pia kua balozi akiwakilisha Zimbabwe nchini Afrika ya Kusini, Botswana pamoja na Urusi

Wakili wa kiongozi huyo, Zibusiso Ncube alisema mteja wake alitoweka baada ya kuhofia kukamatwa na kuwekewa sumu.

Inaelezwa kuwa makamu huyo alikuwa sehemu ya kikundi ambacho kilitaka Neema ambaye ni mke wa Rais Mugabe afanikiwe badala ya Mnangagwa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527