AJALI YA MOTO MOROGORO: LUGOLA AKATISHA ZIARA YAKE MKOANI RUKWA


Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola  ameamua kuahirisha  ziara yake Mkoani  Rukwa  kutokana na ajali ya moto iliyotokea eneo la Msamvu Mjini Morogoro.

Ajali hiyo imetokea leo tarehe 10 Agosti, 2019 majira ya saa 2 asubuhi ambapo lori hilo lililokuwa linatoka Dar es Salaam limepinduka jirani na Kituo Kikuu cha Mabasi cha Msamvu baada ya dereva wa lori kumkwepa mwendesha pikipiki na kisha mafuta yaliyokuwa yakimwagika kushika moto na kuunguza watu waliokuwa wanayachota.

Waziri huyo ameanza safari kuelekea eneo la tukio.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527