STANDARD CHARTERED YATANUA WIGO WA UWEKAJI WA AMANA KWA WATEJA WAKUBWA

 Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bi. Juanita Mramba akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kibenki kwa Makampuni makubwa, ya kati na taasisi za kifedha wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw.  James Meitaron wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa huduma mpya ya fedha kwa wateja wake wakubwa ya kuweka fedha katika akaunti zao kwa kutumia mashine maalumu (Cash Deposit Machines services-CDMs) zitakazowekwa kwenye eneo la kazi uliofanyika Hoteli ya Hyatt-The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja Bidhaa za makampuni makubwa na ya kati wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw. Busara Raymond.
 Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kibenki kwa Makampuni makubwa, ya kati na taasisi za kifedha wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw.  James Meitaron akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu huduma mpya ya fedha kwa wateja wake wakubwa ya kuweka fedha katika akaunti zao kwa kutumia mashine maalumu (Cash Deposit Machines services-CDMs)  zitakazowekwa kwenye eneo la kazi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyika Hoteli ya Hyatt-The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja Bidhaa wa makampuni makubwa na ya kati wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw. Busara Raymond na kulia ni Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bi. Juanita Mramba.
 Meneja Bidhaa wa makampuni makubwa na ya kati wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw. Busara Raymond akizungumza jambo na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa huduma mpya ya fedha kwa wateja wake wakubwa ya kuweka fedha katika akaunti zao kwa kutumia mashine maalumu (Cash Deposit Machines services-CDMs) zitakazowekwa kwenye eneo la kazi  uliofanyika Hoteli ya Hyatt-The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kibenki kwa Makampuni makubwa, ya kati na taasisi za kifedha wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw.  James Meitaron na kulia ni Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa benki hiyo, Bi. Juanita Mramba.
 Baadhi ya mashine maalumu za kuweka fedha (Cash Deposit Machines services-CDMs) zitakazowekwa kwenye  eneo la kazi kabla ya kuzinduliwa rasmi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt-The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.

 Meneja Bidhaa wa makampuni makubwa na ya kati wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw. Busara Raymond (kulia) akitoa maelezo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) jinsi mashine maalumu ya kuweka fedha (Cash Deposit Machines services-CDMs) kwenye eneo la kazi inavyofanyakazi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa huduma mpya ya fedha kwa wateja wake wakubwa uliofanyika Hoteli ya Hyatt-The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kibenki kwa Makampuni makubwa, ya kati na taasisi za kifedha wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw.  James Meitaron.
 Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kibenki kwa Makampuni makubwa, ya kati na taasisi za kifedha wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw.  James Meitaron akikata utepe ishara ya kuzindua rasmi mashine maalumu ya kuweka fedha (Cash Deposit Machines services-CDMs) kwenye eneo la kazi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa huduma mpya ya fedha kwa wateja wake wakubwa uliofanyika Hoteli ya Hyatt-The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Meneja Bidhaa wa makampuni makubwa na ya kati wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw. Busara Raymond pamoja na Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa benki hiyo, Bi. Juanita Mramba.
 Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kibenki kwa Makampuni makubwa, ya kati na taasisi za kifedha wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw.  James Meitaron (kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kuzindua mashine maalumu za kuweka fedha (Cash Deposit Machines services-CDMs) kwenye eneo la kazi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa huduma mpya ya fedha kwa wateja wake wakubwa uliofanyika Hoteli ya Hyatt-The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa benki hiyo, Bi. Juanita Mramba na kulia ni Meneja Bidhaa wa makampuni makubwa na ya kati wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw. Busara Raymond.
 Mpiga picha wa gazeti la Mwananchi, Said Nanjundo akiuliza swali kwa uongozi wa Benki ya Standard Chartered wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa huduma mpya ya fedha kwa wateja wake wakubwa ya kuweka fedha katika akaunti zao kwa kutumia mashine maalumu (Cash Deposit Machines services-CDMs) zitakazowekwa kwenye eneo la kazi uliofanyika Hoteli ya Hyatt-The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kibenki kwa Makampuni makubwa, ya kati na taasisi za kifedha wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bw.  James Meitaron katika picha na moja ya mashine maalumu ya kuweka fedha (Cash Deposit Machines services-CDMs) kwenye eneo la kazi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa huduma mpya ya fedha kwa wateja wake wakubwa uliofanyika Hoteli ya Hyatt-The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.

BENKI ya Standard Chartered jana imezindua huduma mpya ya fedha kwa wateja wake wakubwa, ambao wataweka fedha hizo katika akaunti zao kwa kutumia mashine maalumu (Cash Deposit Machines services-CDMs) zitakazowekwa kwenye eneo la biashara.
Huduma hiyo ni juhudi za benki hiyo kutekeleza matakwa ya wateja wake ya kuwa karibu nao na kurahisisha uwekaji wa fedha na usalama wake.

Huduma hiyo ambayo inawezesha mteja kuwa na mtambo wa kuwekea fedha katika eneo lake la kazi (Cash Deposit Machines services-CDMs) imelenga kwa wafanyabiashara wakubwa kama wenye vituo vya mafuta, maduka makuu, na wauzaji wa vinywaji baridi.
Imeelezwa kuwa CDMs hizo zitafungwa katika maeneo ya biashara hizo na kutoa huduma za kuhifadhi fedha muda wowote ule.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi huo wa huduma za CDMs,  Mkuu wa Kitengo cha huduma za kibenki kwa Mashirika, Biashara na taasisi za kifedha, Bw.  James Meitaron, alisema: “ Benki ya Standard Chartered inazindua Cash Deposit Machines ili kuwezesha wateja wetu wakubwa kuwa na muda zaidi wa kushughulika na kazi na kuacha shaka ya upelekaji wa fedha nyingi kila mara. kwa kuwa na  CDMs wateja wetu sasa wanaweza kuhifadhi fedha katika akaunti zao muda wowote katika mtambo huo. fedha zinazowekwa zitaonesha katika kumbukumbu za kibenki.” 

Aidha alisema kwamba CDMs imeunganishwa na mifumio mingine ya kibenki ya kidigitali ikiwamo Bank’s Corporate Banking Digital platform, S2B, hivyo kumwezesha mteja kuona kinachoendelea katika akaunti yake.

Akizungumzia usalama wa mitambo hiyo, Meitaron alisema kwamba benki inawajibika mara tu fedha hizo zinapowekwa katika mitambo ya CDMs. Pia benki ndiyo itakayosafirisha fedha hizo kutoka katika eneo la mteja hadi benki. 

Mitambo hiyo itawekwa katika maeneo ya mteja yaliyo salama huku hatua zote za kiusalama zikiwa zimetekelezwa.
Pia mitambo hiyo ina uwezo wa kutambua fedha za bandia na kwamba zitakuwa zinaangaliwa na watu ambao watachaguliwa na wateja wenyewe.
“baadhi ya wateja wetu wana huduma hizi na wameomba mitambo zaidi kutokana na haja  kutunza muda na usalama wa fedha. Nashauri wateja wengi  kujaribu huduma hii watafurahi,” alisema Meitaron 

Uzinduzi wa CDMs unafanyika ikiwa ni sehemu ya harakati za benki za kufikia wateja wake pale walipo kwa kutumia njia mbalimbali. Hivi karibuni benki hiyo ilizindua Full Digital Bank on Mobile kwa ajili ya wateja wadogo binafsi na hii ya CDMs ni kwa ajili ya wateja wakubwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527