SIMBA YAMDONDOSHA AJIB ASAINI MIAKA MIWILI


Klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam imefanikiwa kumrejesha nyumbani aliyewahi kuwa mchezaji wake Ibrahim Ajibu Migomba ambaye ametambulishwa hii leo na klabu hiyo kupitia ukurasa wa Instagram. 
Simba imejiwekea utaratibu wa kila siku jumatatu mpaka ijumaa saa saba kamili mchana kutambulisha wachezaji ambao imewasajili kwaajili ya msimu ujao. 

Taarifa ya Simba ambayo imechapishwa katika ukurasa huo wa Instagram inasema kuwa 

Ibrahim Ajib akisaini mkataba.

“Safari ya mtoto kuishi mbali na nyumbani imefikia ukingoni. Ibrahim Ajibu ameamua kufanya maamuzi sahihi ya kurudi nyumbani Msimbazi, ndio amerudi na amesaini mkataba wa miaka miwili kucheza na kuwapa furaha Wanasimba. Karibu nyumbani Ajibu”imesema taarifa hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527