IGP SIRRO AONGOZA KIKAO CHA UTENDAJI CHA MAOFISA WAKUU WA JESHI LA POLISI


Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro (katikati), akiongoza Kikao cha Utendaji cha Maofisa Wakuu  wa Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es salaam, kujadili utendaji wa kazi za Polisi, kufanya tathmini, Mafanikio, Changamoto na kuweka mikakati ya kutekeleza kazi za Polisi hususan kulinda maisha ya raia na mali zao.

Kushoto kwake ni Kamishna wa Kamisheni ya Ushirikishwaji wa Jamii CP Mussa A. Mussa na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo CP Liberatus Sabas na kulia kwake ni Kamishna wa Kamisheni ya Uchunguzi wa Kisayansi CP Shabani Hiki na Kamishna wa Utawala na Rasilimali Watu CP Benedict Wakulyamba.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post