SERIKALI YA CHINA NA TANZANIA KUENDELEZA USHIRIKIANO KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA


Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China imeahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya Malaria ili kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi salama isiyo ya maambukizi ya Ugonjwa huo.


Hayo yamesemwa jana na Naibu Waziri wa Afya kutoka Uchina Mhe. Lin Bin alipotembelea Ikwiriri, Rufiji Mkoa wa Pwani katika mradi wa ushirikiano wa pamoja baina ya China na Tanzania katika kudhibiti ugonjwa wa malaria huku akiongozana na mwenyeji wake Waziri wa Afya,M aendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu.

“China kuwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa kimatafa tutaendeleak ushirikiana kwa pamoja katika kusaidia Tanzania inafikia malengo ya kutokomeza ugonjwa wa malaria” amesema Mhe. Lin Bin na kuendelea kusema Ugonjwa wa malaria unatibika na kuzuilikaW aziri Lin Bin amesema kuwa ushirikiano baina ya Tanzania na China umeleta manufaa katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria kwa kupunguza kiwango cha maambukizi ya ugonjwa huo Wilayani Rufiji kutoka asilimia 25 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 4.9 mwaka 2019.

“Kwa muda wa miaka 60 tumekuwa tukipambana dhidi ya ugonjwa wa malaria ambao umeathiri zaidi ya watu milioni 30, na tangia mwaka 2017 hakuna taarifa zilizolipotiwa kuhusu ugonjwa wa malaria nchini China” amesema Mhe. Lin Bin huku akiipongeza Tanzania kwa mikakati mizuri yenye lengo la kuhakikisha inatokomeza ugonjwa wa malaria.

Kwa upande wake Waziri wa Afya Tanzania, Mhe. Ummy Mwalimu ameishuruku Serikali ya China inayoongozwa na Rais Xi Jinping kwa kuendeleza ushirikiano wa enzi uliopo wa baina ya nchi hizo.

Waziri Ummy amesema kuwa ugonjwa wa malaria bado ni tatizo kubwa sana nchini Tanzania, huku takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO)z ikionyesha kuwa asilimia 55 ya vifo vitokanavyo na malaria vinatoka katika nchini saba za Bara la Afrika ikiwemo Tanzania.

“Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli tumechukua hatu ambali mbali kwa kushirikiana na wadau wakiwemo China kupambana na malaria na yapo mafanikio makubwa ambayo tumeyapata” Amesema Waziri Ummy Mwalimu na kuendelea;
“Tumeweza kupunguza kiwango cha maambukizi ya malaria kutoka asilimia 14.7 mwaka 2015 hadi 7.3 mwaka 2018”.

Amesema kuwa wagonjwa wapya wa malaria wamepungua kwa asilimia 26 kutoka watu 161 katika kila watu 1000 mwaka 2014 hadi kufikia 119k atika kila watu 1000 mwaka 2018 huku vifo vitokanavyo na malaria vimepungua kwa asilimia 55, kutoka vifo 20 katika watu 1000 mwaka 2014 hadi kufikia vifo 9 kati ya watu 1000 mwaka 2018.

“Serikali ya Tanzania itaendela kuchukua hatua kwa kushirikiana na wadau wetu wakiwemo Serikali ya China kuhakikisha tunapunguza kiwango cha maambukizi ya maralia hadi kufikia asilimia 1 ifikapo mwaka 2020” alisema Waziri Ummy Mwalimu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527