Nape Nnauye: " Wakubwa Wananichukia, Wacha Wanichukie maana Napigania Haki za Wananchi"

Mbunge wa jimbo la Mtama (CCM), Nape Nnauye amesema hana kinyongo na serikali yake na kwamba anapigania haki ya wananchi wake kama walivyoahidi kuwasimamia.

Nape alisema awali mbaazi ilikuwa inafanya vizuri sokoni baadaye ikashuka kutoka Sh 2000 hadi Sh 100.

“Ndio maana mbunge wenu nikawa mkali bungeni wapo watu wanasema Nape mkali na wakati mwingine wakubwa wanachukia lakini ninasema bora nichukiwe lakini watu wangu waone nimesimamia haki yao

Aliongezea kuwa:” CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi sina jambo baya na mtu sina kinyongo na serikali yangu lakini tuliwaahidi tutasimamia haki yenu wanaosema Nape anaisemea Kusini yote ndio ni kweli Kusini yote ni maskini.

Nape alisema anatambua nia ya Rais John Magufuli alitaka kuwaokoa kutoka katika bei mbaya akapanga mpango bahati mbaya waliomshauri na waliotekeleza wakalikoroga.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments