MAKAMBA ATOA NENO MRADI WA MAGARI YA UMEME TANZANIA


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba amesema ni lazima athari za usafiri wa magari ya umeme kwenye mazingira ziangaliwe kabla ya huduma hiyo kuanzishwa.


Makamba ametoa mwongozo huo kupitia ukurasa wake wa Twitter kufuatia taarifa ya TANAPA jana Julai 5, 2019 kwamba inajipanga kuleta usafiri wa magari ya umeme ili kurahisisha utalii.

Taarifa ya TANAPA ilieleza hivi, ''Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), inatarajia kuanzisha usafiri mpya wa kutumia magari ya umeme yanayopita kwenye nyaya (Cable Cars), kupeleka watalii Mlima Kilimanjaro''.

Leo Julai 6, 2019 Waziri Makamba amesema ''Inabidi watu wa Mazingira tupitishe na kutoa cheti kwanza kabla hawajaanza. Na tutafanya studies ili kujua impact kwa mazingira na uthabiti wa mitigation measures''.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527