ALIYEKWENDA KUANGALIA NGOMA ZA KIENYEJI AKUTWA AMEFARIKI DARAJANI SHINYANGA



Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao

Mwanaume aliyejulikana kwa jina la Maganga Masunga (42)mkazi wa Kitongoji cha Luhumbo, kijiji cha Galamba kata ya Kolandoto Manispaa ya Shinyanga amekutwa amefariki dunia katika eneo la daraja la barabara itokayo Shinyanga Mjini kuelekea kijiji cha Galamba. 


Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao mwanaume huyo alikutwa amefariki dunia Julai 8,2019 majira ya saa moja usiku

Ameeleza kuwa "kwa mara ya mwisho marehemu aliondoka nyumbani kwake kuelekea kijiji cha Nobora kata ya Ukenyenge wilaya ya Kishapu kwa madhumuni ya kuangalia michezo ya ngoma za kienyeji iliyokuwa inafanyika kijijini hapo Julai 3,2019 saa mbili asubuhi".

Kamanda Abwao amesema chanzo cha tukio hilo kinachunguzwa.
Na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527