Tanzia : MENEJA MAWASILIANO WA SHIRIKA LA AGPAHI AGNES KABIGI AFARIKI DUNIA



Agnes Kabigi enzi za uhai wake
Meneja Mawasiliano wa asasi inayolenga kutokomeza UKIMWI kwa watoto na familia Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI), Bi. Agnes Kabigi (52)amefariki dunia leo mchana Ijumaa Julai 26,2019.
Agnes Kabigi ambaye ni mwandishi Mwandamizi aliyewahi kufanya kazi katika Magazeti ya Uhuru,Mzalendo na Nipashe amefariki dunia baada ya kuanguka ghafla wakati akitekeleza majukumu yake wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Taarifa za kifo cha Agnes Kabigi zimethibitishwa na Mkurugenzi wa Shirika la AGPAHI, Dkt. Sekela Mwakyusa.

"Ni kweli ndugu yetu Agnes Kabigi ametutoka,amefariki dunia huko Kahama baada ya kuanguka akiwa kwenye majukumu ya kikazi" - Dkt. Mwakyusa.

R.I.P AGNES KABIGI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527