RAIS MAGUFULI AMPONGEZA FARU RAJABU..AMPONDA WA JINA WAKE 'JOHN'


Rais wa Tanzania, John Magufuli amesema tangu kuanzishwa kwa kikosi kazi cha kupambana na ujangili mwaka 2016 idadi ya wanyama hapa nchini imeongezeka.

Magufuli amesema hayo leo Jumanne Julai 9 mwaka 2019 wakati wa uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi-Chato mkoani Geita.

"Mwaka 2014 kulikuwa kuna tembo 43,330 lakini hivi sasa baada ya kuanzisha kikosi cha kupambana na ujangili wamefikia zaidi ya 60,000 faru hawakuwepo kabisa ila sasa wamefikia 163 hatuna budi kumshukuru Faru Rajabu mtoto wa Faru John," amesema Magufuli.

"Inaonekana yule Faru wajina wangu (John alikuwa hajitumi vizuri) huyu mtoto wake nimeambiwa mpaka sasa amekwisha zalisha 43," amesema Rais Magufuli huku akitabasamu.
Na Ephrahim Bahemu, Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527