JESHI LA POLISI LAWANASA RAIA 3 WA KIGENI WAKISAFIRISHA MADINI

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu watatu raia wa kigeni kwa kosa la kusafirisha madini aina ya dhahabu bila kuwa na kibali.

Watuhumiwa hao walikuwa wakitokea Wilaya ya Chunya kuelekea Jijini Dar es salaam.Watuhumiwa hao ni 1: Clive Rooney (62)raia wa nchi ya Ireland 2: Ross Stephen Chertsey (34), raia wa nchini Uingereza pamoja na 3:Robert Charles 58, raia wa nchini Uingereza.

Tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 03.07. 2019  huko Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Songwe (SIA), Kata ya Nsalala,Tarafa ya Usongwe Wilaya ya Kipolisi Mbalizi. Watuhumiwa hao walikamatwa na maafisa wa usalama wa uwanja huo wa Songwe.

Madini hayo yalikuwa na uzito wa gramu 1,044.95. Ufuatiliaji unaendelea kufanywa na Kikosi kazi cha kamati ya usalama ya Mkoa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527