WAZIRI WA AFYA AUTAKA UONGOZI WA UWANJA WA NDEGE WA MWANZA KUWEKA MASHINE KWA AJILI YA KUPIMIA UGONJWA WA EBOLA


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ameutaka uongozi wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuweka mashine kwa ajili ya kupimia ugonjwa wa Ebola kwa wasafiri wanaoingia nchini.


Waziri Ummy ametoa maagizo hayo leo Jumamosi Juni 15, 2019 wakati akifanya ukaguzi kwenye uwanja huo kuangalia kama kuna mashine  za kupimia ugonjwa huo ambao umeripotiwa kuibuka nchini Uganda.

Amesema Serikali kupitia  wizara yake watatoa mashine kwenye kivuko cha Busisi, Kigongo na kituo cha mabasi cha Nyegezi jijini humo.

Pia,  kwa wasafiri hao wa mabasi kutoka nchi jirani wanaotumia mikoa ya Kigoma na Kagera.

"Kuwepo kwa Ebola sio tatizo hilo linaweza kuthibitiwa ila tatizo ni kusambaa kwa ugonjwa huo," amesema Waziri Ummy.

Kwa upande wake, kaimu meneja wa uwanja huo, Seneth Lyatuu amesema watatekeleza agizo hilo na wanahitaji mashine mbili kwa ajili ya abiria wa ndani na abiria wa nje.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527