WADUKUZI 'HACKERS' WATEKA TOVUTI ZA SERIKALI NA KUFUTA TAARIFA

Serikali ya Kenya imebaki imeduwaa baada ya ‘hackers’ kupenya kwenye tovuti zake kadhaa na kuchukua usukani.

 Hali ni mbaya hivi kwamba hata mtandao wa kulipia madeni ya serikali maarufu kama IFMIS ulikuwa pia umedukuliwa. 

Kulingana na gazeti la Standard, jumla ya tovuti 27 ya serikali ikiwemo ile ya Huduma ya Vijana kwa Taifa (NYS), IFMIS na mingineyo ilikuwa imetwaliwa na wapenyezi hao kufikia Jumatatu Juni 3,2019. 

 Wale waliokuwa wakijaribu kuingia kwenye mtandao wa IFMIS walikuwa wanajikuta wameingia kwenye tovuti nyingine iliyojiita KURD Eletronic Team.

 Baada ya kundi hilo KURD kuteka tovuti hizo, liliweka logo zake huku likifuta habari za serikali.

 Licha ya kuwa ilikuwa vigumu kuingia kwenye IFMIS kufikia Jumatatu, Juni 3, baada ya shambulio hilo, wizara ya fedha ilisema kuwa mambo yalikuwa salama salmini. 

 “Mtambo wa IFMIS uko sawa. Hakujawa na shambulio lolote kwenye mtambo huu. Kile washambulizi walijaribu ni kuingia kwenye tovuti ya IFMIS, lakini tovuti na mtambo ziko tofauti,” Ujumbe ulisema. 

Tukio hilo ni changamoto kubwa kwa serikali ambayo hivi maajuzi imekuwa ikiokota /taarifa data za wananchi wote huku kukiwa na maswali chungu nzima wa iwapo habari hizo ziko salama.
Chanzo - TUKO

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post