TAIFA STARS KUSHUKA DIMBANI LEO DHIDI YA SENEGAL


Timu yetu ya Tanzania, Stars  leo Jumapili June 23  itachuana na Senegal katika mchezo wa Fainali za Afcon, mechi itakayopigwa saa 2 usiku kwa saa za nyumbani (Tanzania).

Nahodha wa Taifa Satars, Mbwana Samatta amesema kamwe  hawatokubali kufungwa kirahisi katika mchezo huo.

Samatta amesema anajua wanaenda kucheza na timu kubwa yenye wachezaji wanaotazamwa kila wikiendi katika ligi bora lakini hilo haliwatishi wao kupambana katika mchezo huo.

"Tunajua kwamba wapinzani wetu ni wazuri na tunawaheshimu, hatuendi kuwashangaa zaidi na sisi tunaenda kupambana nao na ndio maana tumejiandaa kwa muda mrefu kuweza kupambana," amesema.

Ameongeza anaamini mchezo huo mpaka dakika ya mwisho kila timu ina uwezo wa kupata matokeo uwanjani.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post