TAARIFA UMMA KUHUSU KIKAO CHA KAMATI KUU(CC) NA HALMASHAURI KUU YA TAIFA (NEC) YA CHAMA CHA MAPINDUZI


Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania kinatarajia kufanya vikao vyake Kamati Kuu (CC) pamoja na Halmashauri kuu (NEC) wiki ijayo Dar es Salaam.


Wakati kikao cha kamati kuu vitafanyika Juni 26, 2019 kikao cha NEC kitafanyika Juni 27,2019 na kitakuwa cha kawaida kwa mujibu wa kalenda ya chama na Katiba ya CCM ibara ya 101(2).

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari  Ijumaa Juni 22, 2019 na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole ilisema kikao cha Kamati kuu kikitanguliwa na vikao vya Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa kitakachofanyika Juni 24,2019 na kufuatiwa na semina ya makatibu wa mikoa Juni 25, 2019.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527