TAARIFA MUHIMU KUTOKA WIZARA YA ARDHI

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inawatangazia wananchi wote waliopewa viwanja katika eneo la Pemba Mnazi kukamilisha malipo ya viwanja kabla ya Julai 31 2019.

Kwa wananchi ambao watashindwa kukamilisha malipo kwa muda uliotolewa viwanja vyao vitagawiwa kwa waombaji wengine bila taarifa yoyote. 

Tangazo hili pia litawahusu wale waliolipia sehemu ya gharama za umilikishaji lakini hawajakamilisha malipo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527