SPIKA NDUGAI ATEMBELEA TIMU YA TAIFA STARS NCHINI MISRI


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amekutana jana na wachezaji wa timu ya taifa Taifa Stars katika kambi ya timu hiyo iliyopo nchini Misri.

Katika mazungumzo na wachezaji hao Spika alifikisha ujumbe wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli kuwataka vijana hao kupambana kuhakikisha wanaipeperusha vyema bendera ya taifa katika mashindano ya Afrika yanayotarajia kuanza Juni 21 nchini Misri.

Spika aliwataka wachezaji hao kuingia uwanjani wakiwa wamejua wamebeba matumaini makubwa kwa Watanzania ambao macho na masikio yao wameyaelekeza kwao.

Kwa upande wa nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta alimuahidi Spika kuwa wamepokea salamu za  Rais Magufuli na wamemuahidi kuwa wataingia uwanjani kupambana na kuhakikisha wanaipeperusha vyema bendera ya taifa.

Alisema hawataki kumuahidi kitu kikubwa,ila watajitahidi kadri ya uwezo wao kuhakikisha wanapambana na kupata ushindani katika mechi zote za makundi.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527