MAMA ALIYETELEKEZWA NA MMEWE BAADA YA KUJIFUNGUA MAPACHA WANNE ATUA BUNGENI DODOMA

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.

Mama aliyejifungua watoto Mapacha wanne Radhia Solomon[24] mkazi wa Chemchemi  Magomeni  jijini Dar ES salaam na kutelekezwa na mmewe kwa madai ya kukwepa majukumu leo Juni 3,2019 amewasili bungeni jijini Dodoma ambapo bunge limeridhia kila mbunge wa kiume kumchangia Sh.Laki moja na  kila mbunge wa kike kumchangia Sh.elfu hamsini fedha ambazo zitatumika kumsaidia kujikimu na kuwatunza watoto hao.

Akizungumza leo Juni,3,Bungeni jijini Dodoma Spika wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Job Ndugai amesema  jukumu la utunzaji wa watoto ni la kila jamii hivyo bunge limeamua kufanya mchango huo kwa wabunge ili kumsaidia mama na watoto huku akiwaasa wanaume kuacha tabia ya kutelekeza familia zao.

Ikumbukwe kuwa Radhia Solomon alijifungua watoto mapacha wanne Januari 8,2019 katika  hospitali ya Muhimbili Dar Salaam ,watoto wa kike wawili Faudhia  na Fardhia  pamoja na wa kiume wawili Suleiman na Aiman  ni pacha wanne ambao  kila mmoja alikuwa na mfuko wake wa uzazi  na gharama ya kuwanunulia maziwa ya SMA ya Kopo  ni Sh.Elfu 40 kwa siku  kwani  alipojifungua afya yake haikuwa nzuri kunyonyesha hali iliyosababisha Mmewe kushindwa kumudu gharama na kuwatelekeza .


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post