Breaking : RAIS WA ZAMANI WA MISRI MOHAMMED MORSI AFARIKI DUNIA MAHAKAMANI


Aliyekuwa rais wa Misri, Mohammed Morsi, aliyetimuliwa madarakani na jeshi mnamo 2013 ameaga dunia ghafla akiwa mahakamani, televisheni ya taifa inasema. 

Mahakama nchini Misri ilibatilisha hukumu ya kifo mnamo 2016 dhidi ya rais huyo aliyepinduliwa.

Morsi alikumiwa kifo baada ya kulaumiwa kuhusika na kutoroka kwa wafungwa wengi wakati wa mapinduzi ya mwaka 2011 nchini humo.

Alichaguliwa kuwa rais mwaka 2012 lakini akaondolewa katika mapinduzi ya jeshi mwaka mmoja baadaye, kufuatia maandamano makubwa ya kupinga utawala wake.

Morsi ashahukumiwa kifungo cha maisha jela kwa mashtaka yanayohusu ugaidi.

Tutakujuza zaidi kuhusu taarifa hii kadri tunavyoendelea kupokea maelezo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527