KAULI YA SERIKALI KUHUSU WATUMISHI WA UMMA WANAOJIFUNGUA MAPACHA AU WATOTO NJITI


Serikali  imesema kanuni za kudumu za utumishi wa umma za mwaka 2009 hazijaanisha masharti ya likizo ya uzazi kwa wanawake wanaojifungua mapacha zaidi ya wawili au watoto njiti.

Hayo yameelezwa leo Jumanne Juni 25, 2019 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Mary Mwanjelwa wakati akijibu swali la mbunge wa Viti maalum (Chadema), Anatropia Theonest.

Anatropia amehoji ni muda gani wamekuwa wakipewa wazazi (mtumishi mwanamke au mwanaume) pale wanapopata watoto mapacha zaidi ya wawili au watoto njiti.

“Ikitokea mtumishi wa umma kajifungua watoto mapacha zaidi ya wawili au watoto njiti na kulazimika kuwa na muda zaidi wa kuhudumia watoto hao, mwajiri wake anapaswa kuwasilisha hoja kwa katibu mkuu (utumishi) ili atoe kibali cha kuongeza muda wa likizo ya uzazi. Matukio ya uzazi wa mapacha zaidi ya wawili na watoto njiti ni nadra kutokea mara kwa mara.”

“Natoa wito kwa waajiri na wasimamizi wa rasilimali watu katika utumishi wa umma kutoa taarifa kwa katibu mkuu (utumishi) kuomba kibali cha kuongezwa muda wa likizo ya uzazi kwa watumishi wa umma walio chini yao watakapojifungua watoto pacha zaidi ya wawili au watoto njiti,” amesema Mwanjelwa.

==>Tazama hapo chini


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527