JUMLA YA WASTAAFU ELFU 10, 500 BADO HAWAJAFIKA PSSSF KUHAKIKI TAARIFA ZAO

JUMLA ya wastaafu elfu 10,500 bado hawajafika kwenye ofisi za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), ili kuhakiki taarifa zao hadi sasa, Meneja Kiongozi Uhusiano wa Mfuko huo Bi. Eunice Chiume ameyasema hayo kwa nyakati tofauti wakati akitembelea vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo Juni 11, 2019.

Vyombo vya habari alivyotembelea leo Juni 11, 2019 kwa lengo la kujenga mahusiano na kueleza shughuli za Mfuko huo ambao ni Mpya ni pamoja na magazeti ya serikali yanayomilikiwa na kampuni ya Tanzania Standard News Papers (TSN), Azam Media, wamiliki wa Azam TV na Uhai FM, Mwananchi Communications Limited, wachapishaji wa magazeti ya Mwananchi, Citizen na Mwanaspoti na Clouds Media Group, wamiliki wa Clouds TV na Clouds FM.

Alisema, zoezi la kuhakiki taarifa za wastaafu huwa linafanyika kila mwaka na huu ni utaratibu wa taasisi za hifadhi ya jamii na kwa upande wa PSSSF zoezi lilianza Desemba mwaka jana (2018).

”Tangu Mfuko huu uanze shughuli zake Agosti 1, 2018 PSSSF ilifungua ofisi nchi nzima Bara na Visiwani na hivyo tunatoa wito kwa wastaafu wote ambao bado hawajahakiki taarifa zao kufanya hivyo kupitia ofisi zetu zilizoenea nchi nzima na wala hawalazimiki kuja makao makuu Dodoma kupatiwa huduma hiyo. “Alifafanua Bi. Eunice Chiume.

Zoezi la kuhakiki taarifa hufanyika kila mwaka kwa upande wetu tulianza zoezi hili Desemba mwaka jana (2018) na liliendelea hadi Machi 2019 na tumeanza tena na zoezi hilo nab ado linaendelea.

“kuhakiki taarifa ni muhimu kwani kunasaidia kujiridhisha na taarifa za wastaafu wetu kwa sababu huwa kunakuwa na mabadiliko mbalimbali ikiwa ni pamoaja na kujua kama bado wapo, au taarifa zao za kibenki zimebadilika au la nah ii inasaidia kufanya malipo sahihi na kwa mtu sahihi.” Alibainisha.

Meneja huyo Kiongozi alitoa wito kwa wastaafu na jamii kwa ujumla kuwa PSSSF iko imara katika kuhakikisha inatoa huduma bora kwa wastaafu na wanachama wake wote popote pale nchini. “Mafao yenu yapo wastaafu wote, nendeni mkahakik taarifai, na hata ndugu ambao ndugu zao wastaafu ni wagonjwa wafike kwenye ofisi zetu na sisi tutakwenda kufanya uhakiki huko huko aliko.” Alifafanua Bi. Enice Chiume ambaye anaendelea na ziara yake Jumatano Juni 12, 2019.

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
Kaimu Mhariri Mtendaji wa magazeti ya serikali (TSN), ambaye pia ni Meneja Masoko na Mauzo, Bw, Januarius Maganga(wapili kulia), akizungumza jambo na Meneja Kiongozi Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bi. Eunice Chiume, (wakwanza kushoto), wakati alipotembelea kampuni hiyo jijini Dar es Salaam Juni 11, ikiwa ni ziara ya kujenga mahusiano lakini pia kueleza shughuli za Mfuko huo ambao umeanza kutekeelza majukumu yake Agosti 2018 baada ya serikali kuiunganisha Mifuko minne ya Hifadhi ya Jamii ya PSPF, LAPF, PPF na GEPF.
Meneja Kiongozi Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bi. Eunice Chiume, (wakwanza kushoto), akiwa na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko huo, Bw. Abdul Njaidi (wapili kushoto), wakiwa kwenye mazungumzo na uongozi wa Kampuni ya magazeti ya serikali (TSN), chini ya Kaimu Mhariri Mtendaji, Bw. Januarius Maganga (wakwanza kulia), ikiwa ni muendelezo wa ziara ya meneja huyo kiongzi kutembeela vyombo vya habari kwa nia ya kujenga mahusiano na kueleza shughuli za Mfuko huo mpya.
Meneja Kiongozi Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bi. Eunice Chiume, akifafanua masuala mbalimbali kuhusu shughuli na majukumu ya Mfuko huo.
Meneja Kiongozi Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bi. Eunice Chiume, akifafanua masuala mbalimbali kuhusu shughuli na majukumu ya Mfuko huo.
Kaimu Mhariri Mtendaji wa magazeti ya serikali (TSN), ambaye pia ni Meneja Masoko na Mauzo, Bw, Januarius Maganga, akizungumza mbele ya mgeni wake Bi. Eunice Chiume wakati wa mazungumzo yao
Picha ya pamoja na uongozi wa TSN.
Meneja Kiongozi Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bi. Eunice Chiume, akipeana mikono na Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media, Bw. Tido Mhando, wakati alipotem,belea vyombo vya habari vya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam Juni 11, 2019.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media, Bw. Tido Mhando, (kushoto), akisalimiana na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSSSF, Bw. Abdul Njaidi wakati wa ziara ya kutembelea vyombo vya habari vinavyomilikiwa na kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.
Meneja Kiongozi Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bi. Eunice Chiume(wapili kushoto), na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko huo, Bw. Abdul Njaidi, wakiwa katika mazungumzo na Afisa Mtednaji Mkuu wa Azam Media, Bw. Tido Mhando (wapili kushoto) na Meneja Masoko na Mauzo wa kampuni hiyo, Bw. John Mbele wakati wa ziara ya meneja huyo kwenye vyombo vya habari vinavyomilikiwa na kampuni hiyo vya Azam TV na Uhai FM.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media, Bw. Tido Mhando, akizungumza kwenye mkutano huo.
Meneja Kiongozi Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bi. Eunice Chiume(wapili kushoto), na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko huo, Bw. Abdul Njaidi, (watatu kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na watangazaji mashuhuri wa luninga ya Azam TV, Charles Hillary na Ivona Kamuntu.
Picha ya pamoja
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mwananchi Communications, Bw. Francis Nanai (kulia), akisalimiana na Meneja Kiongozi Uhusiano wa PSSSF, Bi. Eunice Chiume, (wapili kushoto) huku Mhariri Mtendaji wa Kampuni hiyo, Bw. Bakari Machumu akishuhudia wakati wa ziara ya meneja huyo ikiwa ni muendelezo wa kutembelea vyombo vya habari jijini Dar es Salaam Juni 11, 2019.
Mhariri Mtendaji wa gazei la Mwananchi, Bw. Frank Sanga (kulia), akiongozana na Bi. Eunice Chiume, wakati alipotembelea chumba cha habari cha kampuni ya Mwananchi Communications Tabata jijini Dar es Salaam Juni 11, 2019.
Meneja Kiongozi Uhusiano wa PSSSF, Bi. Eunice Chiume, (wapili kushoto) na Bw. Abdul Njaidi (watatu kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na watangazaji wa kipindi cha XXL, cha Clouds FM, kutoka kushoto, B12, Kennedy the Remedy, na DJ
Picha ya pamoja na uongozi wa Clouds Media

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527