MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU APIGWA RISASI AKIRUKA UKUTA AINGIE IKULU NA KISU

Mwanafunzi wa chuo kikuu anauguza majeraha baada ya maafisa wa polisi kumpiga risasi wakati akijaribu kuruka ukuta kuingia Ikulu usiku wa Jumatatu, Juni 10,2019. 

Mwanafunzi huyo wa Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT) kwa jina Brian Kibet Bera, alikuwa amebeba kisu wakati wa tukio hilo.

Brian Kibet, mwanafunzi huyo wa Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT) alikuwa amebeba kisu wakati wa tukio hilo. 

Baadaye Kibet mwenye umri wa miaka 25, ambaye ni mwanafunzi wa somo la uhandisi wa mitambo, alipelekwa katika Hospitali Kuu ya Kenyatta huku uchunguzi ukianzishwa kubaini alichokusudia.

 Polisi wanasema Kibet alipanda kwenye lango na alichomoa kisu baada ya kuamriwa na polisi kujisalimisha na alipokataa, walinzi walimfyatulia risasi begani. 

Baadaye Kibet mwenye umri wa miaka 25, ambaye ni mwanafunzi wa somo la uhandisi wa mitambo, alipelekwa katika Hospitali Kuu ya Kenyatta huku uchunguzi ukianzishwa kubaini alichokusudia. 

Kulingana na ripoti ya polisi, mshukiwa huyo atazuiliwa katika kituo cha Polisi cha Kileleshwa baada ya kutoka hospitalini.

 Mwaka wa 2015, mwanafunzi mwingine Matthew Kinuthia Maina, aliingia Ikulu na kushtakiwa kortini kwa kosa la kuingia katika eneo lenye usalama mkali bila idhini. 

Maina alijitetea kwa kusema kuwa alikuwa na msukumo mkubwa wa kutaka kukutana Rais Uhuru Kenyatta kujadili masuala kuhusu masomo.

 "Kweli niliruka kuingia State House kwa sababu nilijua nitampata rais hapo. Nataka anisaidie na pesa niweze kurekodi muziki wangu ili niweze kupata karo ya shule" Maina aliambia korti wakati akijitetea. 

Via>>Tuko

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527