CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA KAHAMA (KACU) CHATOA ONYO KALI KWA VIONGOZI WA VYAMA VYA MSINGI


SALVATORY NTANDU
Chama kikuu cha Ushirika Kahama (KACU) Katika mkoa wa kitumbaku Kahama, kimekitoza faini ya shilingi laki 300,000  viongozi wa chama cha Msingi Mweli baada ya kubainika kwa mwanachama wake  kubainika  kuchanganya tumbaku safi na Chafu kwenye mabelo yake sokoni kwa lengo la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Hayo yamebainishwa leo na Mwenyekiti wa (KACU) Emanuel Charahani baada ya kubaini tumbaku ya Majaliwa Joseph Masaluta Mkulima na mkazi wa bulungwa katika halmashauri ya Ushetu kufayanya udanganiyifu huo huku viongozi wake wakishindwa kuchukua hatua za haraka kabla ya kuingizwa sokoni.

Amefafanua kuwa Majaliwa  alikuwa na Mabelo  50 yenye zaidi ya kilo 500 ambayo yamebainika kuwa na mchanganyiko wa tumbaku safi na chafu na kwa hatua ya awali ambazo zimekwisha chukuliwa ni pamoja na kuziondoa sokoni tumbaku hizo ili  ukaguzi wakina uweze kufanyika.

Katika hatua nyingine Charahani amesema wakulima waliosajiliwa kulima  zao la tumbaku katika mkoa huo wamelima walikuwa 4,670 na wamelima hekta 5,888 na kuzalisha tumbaku zaidi ya kilo Milioni 8.1 kiwango ambacho ni kikubwa ikilinganishwa na matarajio ya Kampuni zinazonunua zao hilo kwa mkataba.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha ushirika KACU Wilayani hapa Emmanuel Charahani alikili kuwepo kwa vitendo hivyo ambavyo vimekuwa vikijitokeza kila msimu wa uzaji wa tumbaku nakuongeza mwaka huu wamemkamata mkulima mmoja kutoka chama cha msingi Mweli Majaliwa Joseph Masaluta.

Alisema kuwa,alikuwa na tumbaku mabero 50 yenye zaidi ya kilo 500 ambayo yalibainika kuwa na mchanganyiko wa tumbaku safi na chafu na kwa hatua ya awali tumbaku hizo zimeondolewa kwenye soko kwa ajili ya ukaguzi wakina na ikibaika ni mabero yote atafutiwa kibali cha uzalishaji wa zao hilo.

 Hivi karibuni Mkuu wa wilaya ya Kahama Anamringi Macha akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake alizitaka mamlaka zinazosimamia zao hilo ikiwemo bodi ya Tumbaku Tanzania kuchukua hatua kali kwa wakulima wote waytakaobainika kufanya udanganyifu huo ambao unaweza ukasababisha nchi ikakosa mapato kutokana na tumbaku chafu.

Amesema endapo hatua za dharura zisipo chukuliwa na mamlaka husika huenda kampuni zinazoendelea kununua zao hilo hapa nchini zikasitisha kufanya biasha na Tanzania kutokana na kupata hasara inayosababishwa na wakulima wasio waaminifu na kuwataka viongozi wote wa vyama vya msingi kuhakikisha wanasimamia kwa makini suala la ufungashaji wa tumbaku.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527