BUNGE SPORTS CLUB KUTOANA JASHO NA TIMU YA NMB KATIKA UWANJA WA JAMHURI DODOMA LEO


Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania Bunge Sports Club leo Juni 22,2019  wanatimuana Vumbi nene  katika Bonanza la Michezo mbalimbali  na timu ya wafanyakazi Benki ya NMB mchezo  unaocharazwa kuanzia Majira ya  saa 12:00 asubuhi. 


Akizungumza na waandishi wa Habari katika  hafla fupi ya makabidhiano ya jezi za mchezo kutoka NMB Benki Kwenye Ukumbi wa Habari,Bunge, jijiniDodoma meneja wa  timu Ya Bunge Sports  Club  ,Mbunge wa Ulyankulu Tabora  Juma Peter Kadutu  amesema amesema wamejiandaa kuwabamiza vyema NMB na kilichobaki ni kutimuliwa Vumbi tu kwani kila mwaka NMB Wamekuwa  wakifungwa. 


Kadutu ambaye pia ni mwenyekiti wa chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Tabora, na mjumbe wa TFF amesema wana uhakika wa kushinda kwa michezo yote ikiwa ni pamoja na mpira  wa pete na watachukua kikombe. 


Aidha,amesema wanajiandaa na michezo ya wabunge Afrika Mashariki ambayo hufanyika kila Mwaka huku mwaka huu ikitarajiwa kufanyika nchini Uganda huku pia akitumia fursa hiyo kuipongeza Benki ya NMB kwa kuendelea kusapoti kila Mwaka. 


Mkaguzi wa ndani Benki ya NMB makao makuu  Bw.Juma  Kimori amesema Benki ipo sambamba na serikali katika kusaidia masuala ya kijamii. 


Meneja wa NMB kanda ya kati ,Nsolo Mlozi amesema Benki hiyo imejikita kutoa huduma katika maeneo makuu manne katika kusaidia jamii ambayo ni sekta ya  afya,Elimu,elimu  Fedha na kuhudumia jamii katika majanga. 


Aidha,amesema asilimia  1%  ya  mapato hurudi kuhudumia jamii ambapo asilimia 1%  ya mwaka jana zilitengwa zaidi ya Tsh.Bilioni 1 na mpaka sasa zaidi ya Tsh.Milioni 450 zimetumika. 


Michezo inayochezwa katika Bonaza hilo ni pamoja na Mpira wa miguu,mpira wa pete,mpira wa kikapu na Jogging.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527