BABU WA MIAKA 77 AKUTWA AMEKUFA GESTI BAADA YA KUKESHA AKIHONDOMOLA NA MREMBO

Mzee wa miaka 77 nchini Kenya amekutwa amefariki dunia kwenye chumba cha anasa baada ya kukesha na mwanamke mmoja ambaye bado hajatambuliwa.


 Babu huyo aliyejulikana kwa jina la Robert alipatikana uchi wa mnyama kwenye kitanda alichokuwa amejistarehesha na mtoto huyo wa kike. 

Wahudumu kwenye hoteli ya  Kajiado ambapo alipatikana mzee huyo walisema alifika hapo Jumapili, Juni 9,2019 mida ya saa tisa hivi na baada ya kunywa chupa kadhaa za kileo akamchukua mrembo huyo na kuingia kwenye chumba cha malazi. 

Haikubanika kilichofanyika chumbani humo ingawa kulikuwa na dalili za mzee huyo kushiriki penzi na mpenzi wake kwani maafisa wa polisi walipata mipira ya ngono iliyok

Mzee mwenyewe hakuwa na majeraha yoyote huku maafisa wakianza kumsaka binti aliyeingia mitini ili wajue kilicho sababisha mzee kukata roho. 

Mwili wa simba huyo mkongwe ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha City huku ukisubiriwa kufanyiwa upasuaji.
Chanzo - Tuko

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527