Uturuki kununua mfumo wa kujilinda wa Urusi

Waziri wa ulinzi wa Uturuki Hulusi Akar amesema nchi yake inajiandaa kwa vikwazo vya Marekani baada ya kuendelea na mpango wake wa kununua mfumo wa kujilinda na makombora kutoka Urusi. 

Kwenye taarifa iliyosambazwa jana Jumatano, Akar amesema wametuma watu wake nchini Urusi kupewa mafunzo ya kutumia mfumo huo wa S-400, yatakayoanza siku chache zijazo na kuendelea kwa miezi kadhaa. 

Ikulu ya White House ilitishia kuiwekea vikwazo Uturuki, chini ya sheria ya vikwazo inayozuia shughuli za kibiashara na sekta ya intelijensia na ulinzi ya Urusi. 

Marekani, inataraji kuiongezea mbinyo Uturuki, ambayo ni mshirika wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO ili kununua mfumo wa Marekani, lakini Uturuki imekataa kuachana na ununuzi wa mfumo huo wa Urusi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post