SIMBACHAWENE AITAKA SERIKALI IPUNGUZE GHARAMA ZA UMEME


Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene (CCM), amesema gharama za uzalishaji wa umeme kwa sasa ziko juu, hivyo Serikali inatakiwa kuliangalia jambo hilo wakati ikielekea katika uchumi wa kati.

Kauli hiyo ameitoa bungeni leo Jumatano Mei 28, wakati akichangia mjadala wa Wizara ya Nishati kwa mwaka 2019/20.

Aidha, mbunge huyo ambaye amewahi kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, amesema umeme utakuwa na tija kama utaenda katika huduma za kijamii na shughuli za uzalishaji.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527