POLEPOLE: MZEE MENGI ALIKUWA DARAJA KATI YA CCM, SEKTA BINAFSI NA SERIKALI


Katibu Mwenezi wa CCM, Polepole amesema chama chake kinajivunia Mengi kuwa mwanachama wake kwa maelezo kuwa, alikuwa mshauri mkubwa wa masuala ya uchumi na biashara.

Polepole amesema mfanyabiashara huyo alikuwa bilionea mjamaa, alihangaika kuhakikisha kila binadamu anakuwa sawa na mwingine bila kujali hali wala nafasi yake na vilevile ndani ya CCM alikuwa kiungo kati ya chama na Serikali na wadau wa sekta binafsi.

“Alikuwa daraja kati ya sekta binafsi, CCM na Serikali yake, kila panapokuwa na mkwamo kabla mambo hayajaharibika Mzee Mengi alisimama kama kiungo kati ya chama, Serikali na wadau wa sekta binafsi ambao chama chetu kinaamini sana kwamba uchumi wetu unategemea ukuaji na uimara wa sekta hiyo,” amesema.

==>>Msikilize Hapo Chini


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527