JESHI LA POLISI KUMKAMATA ASKOFU GWAJIMA..SAKATA LA VIDEO TATA YA NGONO


Baada ya Video yenye utata inayoashiria kuwa na maudhui ya kingono ambayo inahusishwa na Askofu huyo, Jeshi la Polisi limefunguka kuwa limemuita ajieleze.

Kwa Mujibu wa Kamanda Mambosasa, Askofu Gwajima ameitwa Polisi kwa ajili ya kuhojiwa na ataripoti kesho Mei 8,2019 saa tatu asubuhi

Ameongeza kuwa akichelewa atakamatwa na wamememuita sababu ingawa hakuna aliyelalamika lakini wameona ni kitendo cha ukiukwaji wa maadili, awe Askofu awe Mtu wa kawaida ule ni unyama

“Tayari Askofu Gwajima ameitwa Polisi kwa ajili ya kuhojiwa na ataripoti kesho asubuhi, akichelewa atakamatwa na tumemuita sababu hakuna aliyelalamika lakini tumeona ni kitendo cha ukiukwaji wa maadili, awe Askofu awe Mtu wa kawaida ule ni unyama”,amesema Mambosasa

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527