NEC YAKANA TANGAZO LA AJIRA LA KITAPELI

Tume ya Taifa ya chaguzi inapenda kuutaarifu Umma kuwa, haihusiki na matangazo ya nafasi za ajira yaliyobandikwa katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro.

 
Matangazo hayo yanaeleza kuwa, Tume imetoa ajira za muda, na wananchi walioomba ajira hizo wamekuwa wakiambiwa watoe kiasi cha fedha kwa madai kuwa ni kwa ajili ya mafunzo.

Hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtu au kundi la watu wanaotumia au wanaopanga kutumia jina la Tume ya Taifa ya Uchaguzi kufanya vitendo vya kihalifu.

Tunapenda kuwashukuru wananchi na kuwasihi kuendelea kutoa taarifa mara tu wanapohisi uwepo wa watu au kundi la watu wenye nia mbaya ya kulichafua jina la Tume yaTaifa yaUchaguzi.

Dkt. Athumani Kihamia
MKURUGENZI WA UCHAGUZI


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527