MFUNGO WA RAMADHANI KUANZA KESHO, MEI 7


Kadhi Mkuu wa Tanzania, Abdallah Mnyasi amesema mfungo mtukufu wa ramadhani utaanza kesho Jumanne ya Mei 7, 2019.

Akizungumza jana Jumapili Mei 5,2019 kupitia televisheni ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wakati akifafanua kuhusu mwandamo wa mwezi alisema haujaonekana.

Alisema Waislamu kote nchini wataanza mfungo wa ramadhani mara baada ya kukamilika siku 30 za mwezi Shaaban.

Naye Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum  amesema kwa kushirikiana na Mufti wa Zanzibar, Sheikh Saleh Omar Kaabi,na wa Tanzania Bara, Abubakar Zuber  wamekubaliana mwezi haujaonekana.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527