MBUNGE ADAI UKOSEFU WA MAJI UNAHATARISHA NDOA


Mbunge wa Handeni Vijijini, Mboni Mhita (CCM), amesema ndoa za wanawake wa jimbo hilo zimetetereka kwa sababu wanaamka alfajiri kwenda kuchota maji.

Akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Maji bungeni leo Mei 2, Mboni amesema badala ya wanawake kuhudumia ndoa zao muda huo hutoka kwenda kusaka maji na hivyo kuhatarisha ndoa zao.

“Ndoa nyingi za wanawake wa Handeni Vijijini ziko hatarini wanaamka alfajiri na kushindwa uaminifu, wengine ndoa zao wamezikosa kwa sababu ya kudamka muda huo kwenda kusaka maji na wakati mwingine hurudi bila maji,” amesema Mbunge huyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527