IGP Sirro Afanya Ziara Ya Ukaguzi Kiwanja Cha Ndege Terminal |||

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro (wapili kushoto), akiongozwa na Mhandisi Msimamizi wa Ujenzi wa jengo la kiwanja cha ndege Terminal III Barton Komba, wakati alipofanya ukaguzi wa kuona maendeleo ya mradi huo ambao hadi sasa umekamilika kwa asilimia 99. Picha na Jeshi la Polisi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akitoka kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa kiwanja cha ndege terminal III jijini Dar es salaam, ambapo IGP Sirro alisema Jeshi la Polisi limejipanga kuimarisha usalama kiwanjani hapo. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akikagua gwaride aliloandaliwa kwa ajili yake wakati alipofanya ziara ya ukaguzi katika Kikosi cha Kutuliza Ghasia FFU Ukonga Dar es salaam, ambapo katika ukaguzi wake IGP Sirro alizungumza na maofisa na askari wa kikosi hicho. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro (katikati) akitoa maelekezo kwa maofisa wa Jeshi hilo wakati alipofanya ziara ya ukaguzi katika Kikosi cha Kutuliza Ghasia FFU Ukonga Dar es salaam, kulia ni kamishna wa Operesheni na Mafunzo CP Liberatus Sabas. Picha na Jeshi la Polisi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments