BUNGE LAMLILIA DR. MENGI...SPIKA NDUGAI AELEZEA MCHANGO WAKE


Spika wa Bunge Job Ndugai ametoa taarifa ya Bunge ndani ya ukumbi wa Bunge kuhusu kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa IPP Media Dr. Reginald Mengi kilichotokea Dubai usiku wa kuamkia Mei 2, 2019 ambapo amewaeleza Wabunge kuhusu mchango aliokuwa nao marehemu katika Bunge na taifa kwa ujumla.

"Katika kuomboleza kifo sisi Bunge tunaungana na Mhe. Rais Dkt. John Magufuli, familia ya marehemu na Watanzania wote tukimshukuru Mwenyenzi Mungu na kumshukuru Mhe. Mengi kwa mchango wake mkubwa usiopimika kwetu Watanzania," amesema Spika.

==>>Tazama hapo chini


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527