WANAJESHI 30 WA NIGERIA WATOWEKA KUFUATIA SHAMBULIZI LA BOKO HARAM


Wanajeshi watano wa Nigeria wameuawa na wengine 30 kutoweka kufuatia shambulizi lililofanywa na magaidi wa Boko Haram katika kambi ya wanajeshi hao.


Katika shambulio lililofanywa na magaidi hao jana Jumatatu katika kambi ya wanajeshi hao huko katika mji wa Maiduguri, magaidi walifanikiwa kuiteka kikamilifu kambi hiyo. Kufikia sasa hakuna habari zozote zilizotolewa kuhusiana na hatima ya askari hao waliotoweka.

Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa kufuatia kuongezeka kwa duru mpya ya mashambulio ya magaidi wa Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria, zaidi ya watu elfu 30 katika eneo hilo wamelazimika kukimbia makazi yao na kuishi kama wakimbizi katika maeneo mengine ya nchi hiyo.

Katika mapigano ya miaka 9 ambayo yamekuwa yakiendeshwa kati ya magaidi hao na jeshi la Nigeria, zaidi ya watu elfu 27 wameuawa na wengine milioni moja na laki nane kuwachwa bila makazi na hivyo kusababisha mgogoro mkubwa wa kibinadamu katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527