SERIKALI KUSHIRIKIANA NA UNESCO KUHAKIKISHA USALAMA WA WAANDISHI WA HABARI


Msimamizi wa Usalama wa Waandishi wa Habari wa Wizara ya Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo, Patrick Kipangula akitoa neno la ufunguzi wakati wa kongamano la uandazi wa taarifa ya serikali kuhusu usalama wa waandishi wa habari lililofanyika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Unesco jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Tirso Dos Santos akizungumza wakati wa kongamano la uandazi wa taarifa ya serikali kuhusu usalama wa waandishi wa habari lililofanyika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Unesco jijini Dar es Salaam.
Ofisa programu wa Unesco kitengo cha Habari na Mawasiliano, Nancy Kaizilege akifafanua jambo wakati wa kongamano la uandazi wa taarifa ya serikali kuhusu usalama wa waandishi wa habari lililofanyika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Unesco jijini Dar es Salaam.
Wadau wa tasnia ya habari wakitoa maoni wakati wa kongamano la uandazi wa taarifa ya serikali kuhusu usalama wa waandishi wa habari lililofanyika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Unesco jijini Dar es Salaam.
Ofisa programu wa Unesco kitengo cha Habari na Mawasiliano, Nancy Kaizilege akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wadau wakati wa kongamano la uandazi wa taarifa ya serikali kuhusu usalama wa waandishi wa habari lililofanyika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Unesco jijini Dar es Salaam.
Wadau wa tasnia ya habari walioshiriki kongamano la uandazi wa taarifa ya serikali kuhusu usalama wa waandishi wa habari lililofanyika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Unesco jijini Dar es Salaam. 
Wadau wa tasnia ya habari wakiendelea kujadiliana wakati wa kongamano la uandazi wa taarifa ya serikali kuhusu usalama wa waandishi wa habari lililofanyika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Unesco jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Tirso Dos Santos akifafanua jambo wakati wa kongamano la uandazi wa taarifa ya serikali kuhusu usalama wa waandishi wa habari lililofanyika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Unesco jijini Dar es Salaam.

***
SERIKALI imesema kwamba iko tayari kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na wadau wengine kuhakikisha usalama wa waandishi wa habari wakati wakitekeleza kazi zao.

Kauli hiyo imetolewa Wizara ya Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo wakati wa kongamano la uandazi wa taarifa ya serikali kuhusu usalama wa waandishi wa habari.

Akizungumza kwa niaba ya wizara Msimamizi wa Usalama wa Waandishi wa Habari, Patrick Kipangula alisema kwamba serikali imeweka mazingira sawa ya kumlinda mwandishi wa habari ili kuiwezesha nchi na wananchi kuwa na taarifa za uhakika zinazogusa maisha na maendeleo yao.

Alisema kwamba katika kongamano hilo ni vyema washiriki wake wote wakatazama rasimu hiyo ambayo itakuja kuwasilishwa katika kikao kikubwa cha kitaifa kuzungumzia usalama wa waandishi.

Akizungumzia masuala ya sasa ambapo kukitokea tatizo kuhusu waandishi kunakuwa na malalamiko mengi, alisema kwamba ni vyema ikatambulika kwamba sehemu nyingi duniani na hapa nchini matatizo mengi dhidi ya waandishi wa habari hayasababishwi na serikali bali na watu binafsi.

Alisema waandishi wanapaswa kuelewa sheria wanazofanyia kazi ili kujua haki zao na pia kujua misingi ya usalama wao.

Alisema ni matumaini yake kwamba taarifa hiyo inayopikwa itasaidia kutambua mazingira ya waandishi hapa nchini na kuwezesha kuwa na usalama zaidi kama Umoja wa Mataifa unavyotaka katika kuzingatia vipengele vyake vya maendeleo endelevu hasa kipengele cha 16 na 10 hasa kifungu cha kwanza na cha pili kinachogusa usalama waandishi wa habari na wafanyakazi wa habari.

Alisema kwa sasa serikali imepania kuhakikisha kwamba waandishi wa habari wanakuwa salama na kwamba uhuru wa habari hautishiwi kwa kuwanyima uhuru waandishi wa habari.

Alisema sheria ya vyombo vya habari imetengenezwa kumlinda mwandishi wa habari hasa kwa kuzingatia kwamba waandishi pia wanatakiwa kupelekwa mafunzo na kuwekewa bima.

Katika mkutano huo ambao wawakilishi wa UNESCO walikuwepo, Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Tirso Dos Santos aliwataka washiriki kuchangia ripoti hiyo ili iweze kuwa msingi wa usalama kwa waandishi wa habari.

Alisema taarifa hiyo ambayo pia imetengenezwa kwa taarifa kutoka katika mashirika ya kiraia ni muhimu sana katika utekelezaji wa malengo endelevu ya dunia.

Alisema amefurahishwa sana na juhudi za serikali za kuandika taarifa hiyo, huku akisema mchango wa wadau ni muhimu ili kuwa na ripoti iliyokamilika.

Hii ni mara ya kwanza kwa serikali kuandaa ripoti kwa kusaidiwa na UNESCO kuhusu usalama wa waandishi wa habari ingawa mashirika yasiyo ya kiserikali yamekuwa yakifanya.

Ripoti hiyo ya serikali inatarajiwa kuwasilishwa kwa mamlaka za juu na kujadiliwa Juni mwaka huu, huku taarifa hiyo ikitakiwa kukamilika Mei.

Naye Ofisa programu wa Unesco kitengo cha Habari na Mawasiliano, Nancy Kaizilege alisema katika mkutano huo kwamba ripoti hiyo ni mchanganyiko wa ripoti mbalimbali ikiwamo maswali yaliyoulizwa kwa kupitia mitandao.

Alisema kwamba taarifa hiyo inatarajiwa kufikishwa Wizara ya Fedha kabla ya kwenda kwenye mkutano mkubwa wa wadau.

Alisema kimataifa shauri hilo litakuwa wazi Julai mwaka huu wakati kwa Afrika itakuwa ni juni nchini Morocco.

Katika mkutano huo uliofanyika katika ofisi za UNESCO, wadau walikuwa wanaangalia rasimu ya serikali na usahihi wake kabla ya kwenda kwenye majadiliano katika jukwaa kubwa la kisiasa baadae mwaka huu.

Kwa mujibu wa vipengele vya SDG mataifa wanachama wa Umoja wa Mataifa wanatakiwa kutoa taarifa za hiari kuhusu usalama wa waandishi wa habari na wafanyakazi wa vyombo vya habari.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527