AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA MAKOSA YA KUGHUSHI VYETI VYA TAALUMA

Na Amiri kilagalila
Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa wa Njombe,imemfikisha katika mahakama ya hakimu mfawidhi wilaya ya Makete Bi.HONORATHA MWINUKA katibu muhtasi halmashauri ya wilaya ya Makete na kumfungulia kesi na CC.11/2019 kwa makosa ya kughushi vyeti vya taaluma chini ya sheria ya kanuni ya adhabu kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kaimu mkuu wa Takukuru mkoa wa Njombe CHARLES MULEBYA  amesema kuwa mshtakiwa kwa lengo la kujipatia ajira kama katibu muhtasi alighushi vyeti vya taaluma akionyesha kuwa alisoma kozi ya ukatibu muhtasi katika chuo cha utumishi wa umma (TPSC) Dar es salaam.

Ambapo alihitimu na kupewa cheti cha kumaliza kozi hiyo na kile cha matokeo huku akijua hajawahi kujiunga na chuo hicho wala kuhitimu kozi ya ukatibu muhtasi.

Mulebya amesema kitendo cha mshtakiwa  kughushi vyeti ni kinyume na K/F cha 333,335(a)337 na 342 vyote vya sheria ya kanuni ya adhabu kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Aidha amesema kesi dhidi ya mshtakiwa ipo mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Makete Mh.Jonathan Mpitanjia.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527