TIBA MPYA YA SARATANI YA MATITI YAANZISHWA NCHINI


Mfano wa mwanamke akipima saratani ya matiti.

Wanawake wanaougua saratani ya matiti sasa wamepata ahueni baada ya njia mpya ya tiba ya ugonjwa huo kufanyika pasipo kukata kiungo hicho, baada ya serikali kununua mashine ya tiba za saratani za mionzi inayotumia teknolojia ya kisasa yaani ‘3D’ aina ya Linear Accelerators (LINAC).

Akizungumza na katika hospitali ya Mloganzila leo Aprili 2, 2019 Daktari bingwa wa upasuaji wa matiti kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili , Gasper Haule amesema wanatarajia kufanya upasuaji kwa wagonjwa wanne wanaougua saratani hiyo mapema wiki hii. 

“Tiba hii inafanywa kwa wale ambao wamegundulika kuwa saratani ipo katika hatua ya kwanza na ya pili, tutawafanyia upasuaji, tutatoa vivimbe na kisha watapewa tiba ya mionzi kwa kutumia mashine za kisasa zilizopo Ocean Road,” amesema Dkt. Haule. 

Awali matibabu ya saratani ya matiti yalitolewa nchini kwa njia ya kuondoa kabisa titi katika hatua yoyote ya ugonjwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527