SERIKALI YASEMA HAIJAIZUIA IMF KUCHAPISHA HALI YA UCHUMI WA TANZANIA


Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Phillip Mpango, amesema Serikali haijalizuia Shirika la Fedha Duniani (IMF) kuchapisha ripoti ya uchumi wa Tanzania isipokuwa kinachofanyika ni mazungumzo kati ya serikali ya Tanzania na shirika hilo kabla ripoti hiyo haijachapishwa.

Dk. Mpango ametoa taarifa hiyo bungeni leo Jumanne Aprili 23,2019 alipokuwa akitoa ufafanuzi wa maelezo ya Mbunge wa Tunduma, Frank Mwakajoka (Chadema), aliyesema Serikali imelizuia shirika hilo kutoa ripoti ya uchumi wa Tanzania.

Katika maelezo yake Mwakajoka alipokuwa akichangia makadirio ya bajeti ya Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na  Michezo kwa mwaka wa fedha 2019/20, alisema waandishi wa habari wamejaa hofu ya kuripoti mambo mbalimbali yakiwamo hali ya uchumi wa Tanzania.

Kutokana na hali hiyo alishauri waandishi wa habari waachwe huru ili waripoti mambo mbalimbali kwa maslahi ya umma.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527