RAIS MAGUFULI: MUWEKEZAJI ANAYETAKA KUJENGA ASIHANGAIKE, UKIPATA ARDHI HATA KESHO ANZA KUJENGA


Na. Amiri kilagalila, Njombe
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.John Pombe Magufuli ametoa wito kwa wawekezaji wanaohitaji kujenga kiwanda, kuanza muda wowote pindi watakapopata ardhi bila kusubili huku mambo mengine yakifuata.

Rais ametoa wito huo Mkoani Njombe wakati akizungumza na wananchi Mkoani Njombe mara baada ya kuzindua kiwanda cha kuchakata majani mabichi ya chai cha kabambe kilichopo Lwangu Halmashauri ya Mji wa Njombe Mkoani humo.

“Mtu anapotaka kuja kuwekeza muda mwingine anapata shida masharti ni ya ajabu ajabu na mimi nakubaliana na hilo baadhi ya watendaji wetu wamekuwa ni tatizo katika uwekezaji,wanamuona muwekezaji kama adui badala ya kumuona kama rafiki niwaombe watendaji wangu ndani ya serikali wabadilike,wapo wawekezaji ambao wamekuja hapa wakawekewa mikwara mpaka wakaenda nchi za jirani na wengine wakaombwa rushwa,wengine mara wanafuatwa na Nemc mara kuna Osha vimashariti vya hovyo vimekuwa vingi tunajichelewesha wenyewe”alisema Magufuli

“Sasa nikuombe mheshimiwa waziri na viongozi wengine tubadilike tunatakiwa twende speed nilishazungumza siku moja nilikuwa mkoa wa pwani narudia hapa muwekezaji yeyote anyetaka kujenga chochote asihangaike na mambo mengine yoyote wewe ukishapata eneo hata kesho anza yale mengine yaje baadaye”aliongeza Magufuli

Kwa upande wake, Waziri wa Viwanda,  Joseph Kakunda amesema kuwa kiwanda hicho cha chai kilichozinduliwa hii leo ni miongoni mwa viwanda 36 vya chai nchini ambapo kati ya hivyo viwanda 25 ni vya kusindika majani ya chai na viwanda 11 ni vya kuchanganya majani ya chai kwenye vikasha tayari kwa matumizi.

“Kiwanda hiki cha chai cha kabambe cha uniliver hapa Njombe  ni miongoni mwa viwanda 36 hapa Nchini na kati ya viwanda hivyo ni kiwanda kimoja tu cha Luponde huko Lushoto ambacho hakifanyi kazi tangu mwaka 2013 na tayari tumekirejesha serikalini tumekikabidhi juzi kwa pssf kwa ajili ya kukifufua”alisema Kakunda

Miongoni mwa watu wa waliofanikisha ujenzi wa kiwanda hicho ni pamoja na Rais wa wood foundation Iron wood amesema kuwa jitihada zao za kujenga kiwanda hicho ni pamoja na kuwasaidia wakulima wadogo ambapo mpaka sasa wameweza kuwasaidia wakulima wapatao 3000 wanaoweza kufikisha majani yao ya chai katika kiwanda hicho.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527