RAIS MAGUFULI ATOA MILIONI 10 KUKAMILISHA UJENZI WA WODI YA AKINA MAMA


Na. Amiri kilagalila, Njombe
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dkt. John Pombe Magufuli amekabidhi fedha kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kusaidia kukamilisha ujenzi wa Wodi ya kina mama katika kituo cha afya kifanya kilichopo  halmashauri ya mji wa Njombe mkoani Njombe.

Rais Magufuli  ametoa fedha hiyo mara baada ya kusikia changamoto ya afya inayowakabili wakazi wa kata hiyo, wakati akipokewa huku akitokea mkoani Ruvuma

"Hapa sasa hivi mmenieleza mmejenga kituo chenu cha afya na mmejenga wodi ya akina mama mmeshaezeka ila haijakamilika,mmenifurahisha kwa kuwa mmeanza vizuri hiyo wodi na mimi nawachangia milioni kumi ila zitumike vizuri,nitatuma watu wa kuja kuchunguza hizo milioni kumi zilivyoenda na atakayezila" alisema Magufuli

Aidha Rais Magufuli amesema anahitaji wodi hiyo ikajengwe kwa milioni kumi inatosha jengo hilo la akina mama huku akiagiza Tamisemi namna ya kuwapeleka manesi na madaktari mapema litakapokamilika jengo hilo.

Naye Mbunge wa jimbo la Njombe Mjini, Edward France Mwalongo ameahidi kutoa mifuko 100 ya simenti huku diwani wa kata ya kifanya Nolasco Mtewele akiahidi Kuchangia mifuko mifuko 50 ya saruji kumuunga mkono Rais Magufuli katika kukamilisha ujenzi huo.

Awali Mbunge wa Njombe mjini Edward mwalongo alisema kuwa wananchi hao kwa kushirikiana na halmashauri walijitahidi kuchangia kituo hicho cha afya lakini bado hakijakamilika

"Mh Rais wananchi hawa kwa kushirikiana na halmashauri wamejitahidi sana kuchangia kituo cha afya na kituo chao kinatumika lakini hakijakamilika,wamejenga jengo la upasuaji limeshaezekwa  ndio tunaendelea nalo,wamechanga  milioni 30 na halmashauri kwa mapato ya ndani wamechangia milioni 30" alisema Mwalongo


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527