RAIS MAGUFULI: BILA MKAPA NISINGEKUWA WAZIRI, NA URAIS YAWEZEKANA MSINGENIONA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amesema hatajali maneno ya watu ambao watasema kuwa yeye anajenga miundombinu kwenye Mkoa anaotoka Rais wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa, kwa kuwa anajua alipomtoa.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo akiwa mkoani Mtwara kwenye uznduzi wa Kituo cha Afya Mbonde kilichopo Masasi ambapo

“Watu watasema ninamjengea Mkapa, ndio ni kweli ninamjengea Mkapa kwasababu bila yeye nisingekuwa waziri na inawezekana hata urais nisingepata kwahiyo kumjengea kabarabara tu nishindwe

“Ninafahamu Mkapa alinitoa wapi, yako maeneo ya barabara hii kilomita 40 mimi nimeyajua kuliko watu wa Mkoa huu kwasababu Mkapa alikuwa ananituma kwenda kufanya kazi.

"Tulipomaliza ujenzi wa daraja la Mkapa tulimwambia tunalipa jina lake akakataa lakini siku anaenda kulizindua alikuta tumeandika jina lake sasa hivi ana miaka karibu 80 haiwezekani kila anapokwenda mahali walipozikwa wazazi wake tushindwe kutengeneza barabara"


Kuhusiana na Waziri wa awamu ya tatu kupewa kiwanda cha korosho lakini hakiendelezi Rais Magufuli amesema; "kuna kiwanda naambiwa ni cha Waziri wa awamu ya tatu mumnyang'anye, akikataa shikeni pelekeni mahakamani hata kama alikuwa Waziri, tukibembelezana hatutafika ndugu zangu, tubembelezane mimi nikishamaliza muda wangu."

"Nitoe wito kwa waliouziwa viwanda vya kubangua Korosho na Serikali, ni lazima waanze kubangua Korosho na wazinunue, wakishindwa wavirudidhe viwanda, mfano yule wa Newala kiwanda hakifanyi kazi kabisa Waziri wa Kilimo mnyanganye hata kama ni leo." amemalizia Rais Magufuli


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527