RAIS MAGUFULI AIBUA KASHFA YA STAMPU HEWA ZA BILIONI 10 TRA


Rais Magufuli amesema Wahujumu uchumi wamewahi kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutengeneza stampu hewa za Bilioni 10.


Amesema stampu hizo baada ya kutengenezwa zilisambazwa katika viwanda nchini kupitia ushirikiano wa baadhi ya wafanyakazi wa TRA.


Kauli hiyo ameitoa jana Jumanne Aprili 9, 2019 akifungua kiwanda cha majani ya Chai katika kijiji cha Kabambe mkoani Njombe, ikiwa ni sehemu ya ziara yake kwenye mikoa mbalimbali nchini.



“Kwenye suala hili la kodi hasa kwenye vinywaji kama vile bia, konyagi na spirit (vinywaji vikali) nyingine hili kidogo ni very complex (linachanganya) ndio maana Mwenyekiti hakuzungumza tulikuwa tunakusanya kiasi gani, angezungumza hilo tungekuwa tunagonga stampu tungekuwa tunakusanya ngapi, tungepata jibu vizuri.

“Hatukusanyi kitu katika eneo ambalo tumepigwa sana ni hilo la vinywaji, kwa hiyo Serikali inakosa pesa hakuna mahali tulipata pesa, lazima sasa tutafute utaratibu mzuri ili hawa wenye viwanda vya vinywaji tusipoteze pesa zaidi” Alisema Rais Magufuli


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527