MVULANA WA MIAKA 16 AWAPACHIKA MIMBA WASICHANA WATATU

Mvulana mwenye umri we miaka 16 kutoka Kibera, Nairobi anadaiwa kuwapachika mimba wasichana watatu. 

Wasichana hao wa umri mdogo kutoka mtaa wa Kibera, Nairobi huenda wakakosa masomo yao kwa muda baada ya mvulana rafiki yao mwenye umri wa miaka 16 kuwatunga mimba katika kipindi cha miezi sita.

 Urafiki wa wasichana hao wa kati ya umri wa miaka 13 na 15 na mvulana huyo ulianza mwishoni mwa 2018 na mapema 2019 na baada ya muda mfupi walipachikwa mimba.



 Katika mahojiano na NTV, Jumamosi, Machi 30, mmoja wa wasichana hao alisema alikutana na baba ya mtoto wake wakati wa kupigwa picha na hatimaye wakaanza urafiki. 

"Baada ya kukutana naye tulianza kupendana. Baada ya mwezi mmoja na nusu niligundua mimi ni mjamzito. Baadaye alikana kuhusika nilipomuuliza," alisimulia. 

Kwa mshtuko mkubwa, msichana huyo we Kidato cha Kwanza aligundua mvulana huyo alikuwa na wasichana wengine wawili ambao tayari nao walikuwa wajawazito. 

Kwa msichana mwingine mwenye umri wa miaka 13, kisa chake kilikuwa tofauti kwani zawadi za mara kwa mara zilimfanya kupumbazwa kimapenzi ingawa hakumpenda mvulana huyo mwanzoni.

Kulingana na takwimu za punde kuhusu visa vya mimba za mapemba miongoni mwa wasichana vi vya juu zaidi Kaunti ya Narok huku ikiongoza kaunti zingine kwa 40%.

 Homa Bay inafuatia kwa 33%, Pokot Magharibi kwa (29%), Mto Tana na Nyamira (28%) kisha nambari sita ni Samburu kwa 26%. 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527