MAHAKAMA YAZUIA KUCHORA VIBONZO VYA KUMKEJELI RAIS


Mahakama Kuu nchini Rwanda imetupilia mbali mashtaka yaliyokuwa yametolewa na baadhi ya wanasheria nchini kupinga sheria iliyoanzishwa mwaka jana kuwa ni kosa la jinai kuchora vibonzo vinavyomkejeli Rais wa nchi hiyo.


Wanasheria hao walifungua kesi kulipinga hilo huku wakisema hiyo ilikuwa ni kinyume cha katiba ya nchi hiyo. 

Hata hivyo mahakama hiyo imeamua kuwa viongozi wengine waandamizi serikalini na viongozi wakuu wa kidini halitakuwa kosa la jinai kuwachora kwenye vibonzo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post